KIPIMO CHA UJAUZITO (UPT)
Kipimo cha ujauzito hutumika
kuthibitisha kama mwanamke ana
ujauzito baada ya kuwa na dalili ambazo
zinaashiria kuwepo kwa
ujauzito, hiki kipimo hupima uwepo wa hormone ya HCG
katika
aidha mkojo au damu ya mama mjamzito, ambapo hii hormone
hutolewa mwilini pale tu mwanamke
akiwa mjamzito takribani siku
6-10 baada ya mimba kutungwa.
Kama mwanamke hana ujauzito basi hormone ya HCG
huwa
haipatikani kwenye damu na mkojo wa mwanamke, lakini akiwa
mjamzito
hormone ya HCG hupatikana aidha kwenye mkojo au
damu ya mama mjamzito.
Ukitaka kupima ujauzito mkojo
au damu huchukuliwa, kwa njia ya
mkojo, mkojo huchukuliwa na kuwekwa kwenye
chombo safi
baadae kipimo huwekwa kwenye chombo chenye mkojo kwa muda
wa
sekunde 10-15 baadae hutolewa kwa kusoma majibu. Kupima
ujauzito kwa njia ya
damu, hii njia hufanyika maaabara tu.
Kipimo huwa na mistari miwili
ambapo kikichora mstari mmoja
huashiria hakuna ujauzito na kikichora mistari
miwili huashiria
uwepo wa ujauzito.
Muda muafaka wa kutumia hiki
kipimo ni pale tu mwanamke
anapogundua kuwa amekosa damu zake za mwezi na ni
vizuri
kupima mapema au wiki moja baada ya kufanya tendo la ndoa,
majibu
yakitoka negative wakati kuna dalili za ujauzito na hakuna
hedhi kuna haja ya
kurudia tena kipimo baada ya siku saba.
Kipimo cha kupima mimba kwa
kutumia mkojo kinapatikana
kwenye maduka ya dawa muhimu na hujulikana kwa jina
la UPT.
Na hutumika mara moja tu.
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO
REFERENCES
D.C.DUTTA,(2011) Text book of
obstetrics, seventh edition, New central book agency(P) ltd, LONDON
GORDON W.GARLAND and ROSEMARY
C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english universities press ltd, LONDON.
LINDA K. BROWN and V.RUTH
BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill
livingstone, EDINBURGH LONDON
No comments