DALILI ZA YAI KUTOKA KWENYE OVARY NA KUWA TAYARI KWA UCHAVUSHWAJI


Si kila mwanamke hupata dalili au viashiria vya yai kutoka kwenye 

ovary, kuna baadhi hupata na wengine hawapati kabisa, na dalili hizi 

na viashiria haviwapati wanawake kwa muda unaofanana kila mtu 

hupata kwa wakati wake na kila mtu ana siku yake peke ake ya yai 

kutoka.
                       
Ni vizuri kuzijua na kuzitambua dalili hizi kwa ajili ya kujua haswa 

lini yai linakuwa linatoka au limetoka na tayari kwa uchavushwaji, 

hii husaidia katika kupanga kwa hiari siku ya kupata ujauzito au 

kupanga kutopata ujauzito, hivyo ni muhimu kufahamu dalili hizi.

Ufahamu wa dalili hizi,  ufahamu wa mzunguko wa hedhi husaidia 

kupanga ni wakati gani mwanamke anahitaji kupata ujauzito au ni 

wakati gani hahitaji kupata ujauzito.


       Picha ikionyesha mzunguko  wa hedhi na matukio yake


Baadhi ya dalili za yai kutoka ni;
Ø 1. Kupatwa na maumivu kama vichomi sehemu za nyonga katikati ya siku za mzunguko wa hedhi

Ø 2. Matone ya damu kutoka kwenye uke katikati ya mzunguko wa hedhi

Ø 3. Matiti kujaa katikati ya mzunguko wa hedhi

Ø 4. Kupata mvurungiko wa tumbo katikati ya mzunguko wa hedhi

Ø 5. Kupatwa na ongezeko la hamu ya kufanya tendo la ndoa katikati ya mzunguko wa hedhi.

Ø 6. Kuongezeka kwa ute wa ukeni

Ø 7. Kutokwa na ute wa ukeni muda wote na ute kubadilika kuwa kama tui jeupe la yai.

Ø 8. Joto la mwili kuongezeka.

IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO
REFERENCES

D.C.DUTTA, (2011) Text book of obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON

GORDON W.GARLAND and ROSEMARY C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english  universities press ltd, LONDON.

LINDA K. BROWN and V.RUTH BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill livingstone, EDINBURGH LONDON

BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD, CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc GrawHill Education, UNITED STATES





No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.