DALILI ZA YAI KUTOKA KWENYE OVARY NA KUWA TAYARI KWA UCHAVUSHWAJI
Si kila mwanamke hupata dalili
au viashiria vya yai kutoka kwenye
ovary, kuna baadhi hupata na wengine
hawapati kabisa, na dalili hizi
na viashiria haviwapati wanawake kwa muda
unaofanana kila mtu
hupata kwa wakati wake na kila mtu ana siku yake peke ake
ya yai
kutoka.
Ni vizuri kuzijua na
kuzitambua dalili hizi kwa ajili ya kujua haswa
lini yai linakuwa linatoka au
limetoka na tayari kwa uchavushwaji,
hii husaidia katika kupanga kwa hiari siku
ya kupata ujauzito au
kupanga kutopata ujauzito, hivyo ni muhimu kufahamu
dalili hizi.
Ufahamu wa dalili hizi, ufahamu wa mzunguko wa hedhi husaidia
kupanga
ni wakati gani mwanamke anahitaji kupata ujauzito au ni
wakati gani hahitaji
kupata ujauzito.
Picha ikionyesha mzunguko wa hedhi na matukio yake
Baadhi ya dalili za yai kutoka ni;
Ø 1. Kupatwa na maumivu kama vichomi sehemu za nyonga
katikati ya siku za mzunguko wa hedhi
Ø 2. Matone ya damu kutoka kwenye uke katikati ya
mzunguko wa hedhi
Ø 3. Matiti kujaa katikati ya mzunguko wa hedhi
Ø 4. Kupata mvurungiko wa tumbo katikati ya mzunguko
wa hedhi
Ø 5. Kupatwa na ongezeko la hamu ya kufanya tendo la
ndoa katikati ya mzunguko wa hedhi.
Ø 6. Kuongezeka kwa ute wa ukeni
Ø 7. Kutokwa na ute wa ukeni muda wote na ute
kubadilika kuwa kama tui jeupe la yai.
Ø 8. Joto la mwili kuongezeka.
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR
MLALO
REFERENCES
D.C.DUTTA, (2011) Text book of
obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON
GORDON W.GARLAND and ROSEMARY
C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english universities press ltd, LONDON.
LINDA K. BROWN and V.RUTH
BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill
livingstone, EDINBURGH LONDON
BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD,
CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc
GrawHill Education, UNITED STATES
No comments