MUDA MUAFAKA WA KUANZA KUFANYA MAPENZI BAADA YA KUJIFUNGUA


Mwanamke anapokuwa mjamzito hupata mabadiliko mbalimbali  

ambayo baadhi hutoweka mara baada tu ya kujifungua, mama 

mjamzito baada ya kujifungua humchukua takriban wiki sita baadhi 

ya viungo vyake hususani vya uzazi kurudi kawaida kama kabla 

hajapata ujauzito, hivyo basi mama mjamzito baada ya kujifungua 

anatakiwa akae takribani wiki sita sawa na mwezi mmoja na nusu 

ndiyo anaruhusiwa kuanza kufanya mapenzi, huo ndo ushauri wa 

kitabibu kwa suala la muda upi sahihi wa kuanza kufanya mapenzi 

baada ya kujifungua. lakini si lazima kuanza kufanya mapenzi baada 

ya huo muda kama familia mnaweza kukubaliana muda wenu rasmi 

wa kuanza kufanya mapenzi lakini usiwe mapema kabla ya wiki sita 

toka mamamjamzito amejifungua.








Kabla ya wiki sita kupita mama aliyetoka kujifungua huwa yuko 

katika kipindi cha mpito ambapo hupata baadhi ya mabadiliko 

katika mwili wake ili aweze kurejea kama alivyokuwa kabla ya 

kupata ujauzito, katika kipindi hiki mama aliyetoka kujifungua 

hutokwa na uchafu ukeni ulio katika hali ya damu hivyo kuwa 

katika mazingira magumu ya kufanya mapenzi.
                       
Pia katika kipindi hiki viungo vya uzazi hujaribu kurudi katika hali 

yake ya kawaida, pia ni kipindi ambacho kwa wale walioongezewa 

njia au waliochanika kwenye uke,  ndo huanza kupona na kurudi 

kawaida, hivyo ni wakati mgumu sana kwa mama alietoka 

kujifungua kuanza kufanya mapenzi katika hiki kipindi.
                       
Pia katika hiki kipindi ni vyepesi sana kwa mama aliyetoka 

kujifungua kupata maambukizi kama hatazingatia usafi na kuanza 

kufanya mapenzi kwa kipindi alichopo.
                               
Pia mama aliyetoka kujifungua viungo vyake vya uzazi kama vile 

uke kabla ya muda wa wiki sita huwa havijapona ipasavyo kiasi cha 

kumfanya apate maumivu kama atafanya mapenzi mapema kabla ya 

muda wa wiki sita, pia kwa mama anayenyonyesha sehemu zake za 

siri huwa kavu kiasi cha kumfanya kupata maumivu endapo 

ataamua kufanya mapenzi mapema.
                         
Hata baada ya wiki sita kuisha mama aliyetoka kujifungua 

anaruhusiwa kuanza kufanya mapenzi hivyo basi anatakiwa pia 

kuwa ameshachagua njia ya uzazi wa mpango kwani anaweza pata 

ujauzito kwa muda wowote atakapoanza kufanya mapenzi, kama 

familia ni vizuri kutambua, kuamua na kupanga njia sahihi ya uzazi 

wa mpango watakayo tumia baada ya mamamjamzito kujifungua. 

Onana na watoa huduma wa afya kwa ushauri mzuri juu ya njia 

sahihi ya uzazi wa mpango.

IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO AFISA MKUNGA

REFERENCES

D.C.DUTTA, (2011) Text book of obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON

GORDON W.GARLAND and ROSEMARY C. PERKES, (1959) a text book for pupil midwives, The English universities press ltd, LONDON.

LINDA K. BROWN and V.RUTH BENNETH, (1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, Churchill Livingstone, EDINBURGH LONDON

BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD, CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc GrawHill Education, UNITED STATES


No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.