MUDA MUAFAKA WA KUANZA KUFANYA MAPENZI BAADA YA KUJIFUNGUA
Mwanamke anapokuwa mjamzito
hupata mabadiliko mbalimbali
ambayo baadhi hutoweka mara baada tu ya
kujifungua, mama
mjamzito baada ya kujifungua humchukua takriban wiki sita
baadhi
ya viungo vyake hususani vya uzazi kurudi kawaida kama kabla
hajapata
ujauzito, hivyo basi mama mjamzito baada ya kujifungua
anatakiwa akae takribani
wiki sita sawa na mwezi mmoja na nusu
ndiyo anaruhusiwa kuanza kufanya mapenzi,
huo ndo ushauri wa
kitabibu kwa suala la muda upi sahihi wa kuanza kufanya
mapenzi
baada ya kujifungua. lakini si lazima kuanza kufanya mapenzi baada
ya
huo muda kama familia mnaweza kukubaliana muda wenu rasmi
wa kuanza kufanya
mapenzi lakini usiwe mapema kabla ya wiki sita
toka mamamjamzito amejifungua.
Kabla ya wiki sita kupita mama
aliyetoka kujifungua huwa yuko
katika kipindi cha mpito ambapo hupata baadhi ya
mabadiliko
katika mwili wake ili aweze kurejea kama alivyokuwa kabla ya
kupata
ujauzito, katika kipindi hiki mama aliyetoka kujifungua
hutokwa na uchafu ukeni
ulio katika hali ya damu hivyo kuwa
katika mazingira magumu ya kufanya mapenzi.
Pia katika kipindi hiki viungo
vya uzazi hujaribu kurudi katika hali
yake ya kawaida, pia ni kipindi ambacho
kwa wale walioongezewa
njia au waliochanika kwenye uke, ndo huanza kupona na kurudi
kawaida, hivyo ni
wakati mgumu sana kwa mama alietoka
kujifungua kuanza kufanya mapenzi katika
hiki kipindi.
Pia katika hiki kipindi ni
vyepesi sana kwa mama aliyetoka
kujifungua kupata maambukizi kama hatazingatia
usafi na kuanza
kufanya mapenzi kwa kipindi alichopo.
Pia mama aliyetoka kujifungua
viungo vyake vya uzazi kama vile
uke kabla ya muda wa wiki sita huwa havijapona
ipasavyo kiasi cha
kumfanya apate maumivu kama atafanya mapenzi mapema kabla ya
muda wa wiki sita, pia kwa mama anayenyonyesha sehemu zake za
siri huwa kavu
kiasi cha kumfanya kupata maumivu endapo
ataamua kufanya mapenzi mapema.
Hata baada ya wiki sita kuisha
mama aliyetoka kujifungua
anaruhusiwa kuanza kufanya mapenzi hivyo basi
anatakiwa pia
kuwa ameshachagua njia ya uzazi wa mpango kwani anaweza pata
ujauzito kwa muda wowote atakapoanza kufanya mapenzi, kama
familia ni vizuri
kutambua, kuamua na kupanga njia sahihi ya uzazi
wa mpango watakayo tumia baada
ya mamamjamzito kujifungua.
Onana na watoa huduma wa afya kwa ushauri mzuri juu
ya njia
sahihi ya uzazi wa mpango.
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR
MLALO AFISA MKUNGA
REFERENCES
D.C.DUTTA, (2011) Text book of
obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON
GORDON W.GARLAND and ROSEMARY
C. PERKES, (1959) a text book for pupil midwives, The English universities
press ltd, LONDON.
LINDA K. BROWN and V.RUTH
BENNETH, (1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, Churchill Livingstone,
EDINBURGH LONDON
BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD,
CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc
GrawHill Education, UNITED STATES
No comments