FAHAMU KUHUSU P2

  •  P2- Ni njia ya uzazi wa mpango inayotumika katika hali ya dharura, hivyo kuitwa njia ya dharura ya uzazi wa mpango. hufahamika pia kama morning after pills, emergency contraceptives, plan B.

                      

  • Njia hii ya uzazi wa mpango huzuia mimba kutungwa na sio njia ya kutoa mimba, hivyo matumizi yake yanatakiwa yatumike kipindi cha dharura tu na sio kama njia ya kutoa mimba au njia za kawaida za uzazi wa mpango.
  • P2 kama njia zingine za uzazi wa mpango zenye vichocheo (hormone), hutumia vichocheo hivi (hormone) kuzuia mimba (implantation) na kuzuia uchwavushwaji wa yai (ovulation). tofauti kati ya P2 na njia zingine za uzazi wa mpango ni kwamba P2 inatumika kwenye mazingira ya dharura wakati njia zingine za uzazi wa mpango zinatumika kila siku au kila miezi na miaka ili kuzuia mimba.
  • mazingira ya dharura ambayo P2 inaruhusiwa kutumika ni kama vile;

1. mwanamke aliyebakwa na hataki kushika ujauzito wa mbakaji

2. kupasuka au kuchomoka kwa condom na shahawa kuingia kwenye uke

3.kufanya tendo la ndoa katika siku za kushika mimba bila kutumia njia yoyote ya uzazi wa mpango

4. mtumiaji wa vidonge vya uzazi wa mpango kusahau kumeza vidonge kwa siku tatu (3) mfululizo na akafanya tendo la ndoa.

  • P2 ikitumika mapema baada ya dharura kutokea huweza kuzuia mimba.


WASILIANA NASI KWA UFAHAMU ZAIDI +255757599024-what's app.

No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.