SARATANI YA MLANGO WA UZAZI.
Ni saratani ambayo hutokea na
kuanzia kwenye shingo ya uzazi ya
mwanamke ambayo isipogundulika na kutibiwa
mapema husambaa
katika viungo mbalimbali vya mwili na huweza sababisha kifo kwa
mama alie na hio saratani.
Saratani hii husababishwa na
kirusi aitwaye human papilloma virus
(HPV) ambaye hupatikana kwenye maumbile ya
kiume au viungo
vya uzazi vya kiume(uume), hiki kirusi huweza kusambazwa kwa
njia ya kujamiana, sana sana kujamiana bila kutumia kinga yoyote
ile yaani
kushiriki ngono zembe katika umri mdogo.
Hiki kirusi kwa mwanaume
hakina madhara na kinaishi kwenye
viungo vyake vya uzazi, madhara kwa mwanamke hutokea
pale tu
kinapokuwa kwenye maumbile ya uzazi ya kike (mlango wa uzazi)
ila kwa
mwanaume wanaweza kupata madhara yanayosababishwa
na hiki kirusi kwa wale
wanaume waliokwenye mahusiano ya jinsia
moja na kushiriki ngono kwa njia ya mdomo
ambapo wakipata
maambukizi ya hiki kirusi huweza kupata saratani ya koo la
hewa.
Saratani ya mlango wa uzazi
inatibiwa pale tu inapogudulika
mapema
na kabla haijasambaa kwenye viungo mbalimbali vya
mwili, maambukizi
huanza kwenye mlango waa uzazi mengine
huweza kupotea bila matibabu yoyote yale
lakini mengine huweza
kuendelea na yasipo gundulika mapema na kupatiwa matibabu
huwa
saratani na baadae kusambaa mwilini mwisho husababisha kifo.
Habari nzuri kuhusu saratani ya
mlango wa uzazi ni kwamba ina
chanjo, inatibika na inagundulika mapema kama mtu
akifanyiwa
uchunguzi na huduma ya uchunguzi inapatikana katika hospitali
kubwa
kama vile KCMC, MUHIMBILI NA BUGANDO. Ni vizuri
kufanya uchunguzi mapema hata
kama huna dalili za saratani hii.
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR
MLALO AFISA MKUNGA (BSc MIDWIFERY)
REFERENCES;
Gynecology by ten teacher 18th
edition
No comments