SARATANI YA SHINGO YA UZAZI.
- Ni saratani ambayo hutokea na kuanzia kwenye shingo ya uzazi ya mwanamke ambayo isipogundulika na kutibiwa mapema husambaa katika viungo mbalimbali vya mwili na huweza sababisha kifo kwa mama alie na hio saratani.
- Saratani hii husababishwa na kirusi aitwaye human papilloma virus (HPV) ambaye hupatikana kwenye maumbile ya kiume au viungo vya uzazi vya kiume(uume), hiki kirusi huweza kusambazwa kwa njia ya kujamiana, sana sana kujamiana bila kutumia kinga yoyote ile yaani kushiriki ngono zembe katika umri mdogo.

- Hiki kirusi kwa mwanaume hakina madhara na kinaishi kwenye viungo vyake vya uzazi, madhara kwa mwanamke hutokea pale tu kinapokuwa kwenye maumbile ya uzazi ya kike (mlango wa uzazi) ila kwa mwanaume wanaweza kupata madhara yanayosababishwa na hiki kirusi kwa wale wanaume waliokwenye mahusiano ya jinsia moja na kushiriki ngono kwa njia ya mdomo ambapo wakipata maambukizi ya hiki kirusi huweza kupata saratani ya koo la hewa.
- Saratani ya mlango wa uzazi inatibiwa pale tu inapogudulika mapema na kabla haijasambaa kwenye viungo mbalimbali vya mwili, maambukizi huanza kwenye mlango waa uzazi mengine huweza kupotea bila matibabu yoyote yale lakini mengine huweza kuendelea na yasipo gundulika mapema na kupatiwa matibabu huwa saratani na baadae kusambaa mwilini mwisho husababisha kifo.
- Habari nzuri kuhusu saratani ya mlango wa uzazi ni kwamba ina chanjo, inatibika na inagundulika mapema kama mtu akifanyiwa uchunguzi na huduma ya uchunguzi inapatikana katika hospitali kubwa kama vile KCMC, MUHIMBILI NA BUGANDO. Ni vizuri kufanya uchunguzi mapema hata kama huna dalili za saratani hii.
WASILIANA NASI KWA UFAHAMU ZAIDI +255757599024-what's app.


No comments