VITU VYA KUFANYA NA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUNGU
Uchungu ni kipindi kigumu kwa
mamamjamzito na ni kipindi
ambacho mwanamke yeyote aliyekwisha jifungua hawezi
kukisahau
katika maisha yake, katika kipindi hiki cha uchungu ni kipindi
kinachohitaji, mahusiano mazuri kati ya mamamjamzito na mtoa
huduma wa afya,
mawasiliano mazuri na ushirikiano wa kutosha
kati ya hawa watu ni vitu muhimu
katika kipindi hiki cha uchungu,
mama mjamzito anatakiwa awe mwerevu, msikivu na
anaetoa
ushirikiano wa kutosha kwa mtoa huduma ya afya anayemsaidia
katika
kipindi cha uchungu.
Hivyo bhasi ili kipindi hiki
kigumu kiweze kuwa chepesi na cha
kusaidika mamamjamzito hana budi kufanya au
kuzingatia vitu
vifuatavyo katika kipindi cha uchungu ili mambo yaweze kuwa
mepesi
· 1. Kufanya mazoezi kama vile kutembea, kwenda na
uchungu chini ( uchungu ukija chuchumaa chini)
· 2. Kunywa chai ya moto yenye sukari nyingi kwa
ajili ya nguvu.
· Kula vitafunwa kama vipo
· 3. Kuhema(kutoa hewa nje) kila uchungu unapokuja
· 4. Kusikiliza unachoambiwa na kuelekezwa na mkunga/daktari
· 5. Si kila mama
mjamzito anapopata uchungu unatakiwa asukume, anatakiwa asubiri mpaka pale atakapopewa
amri ya kusukuma
· 6. Kutokubana miguu wakati wa kusukuma
· 7. Kutokusukuma kabla hajapewa amri ya kusukuma, mama
mjamzito anatakiwa asukume pale tu anapoambiwa asukume
· 8. Wakati wa
kusukuma, mama mjamzito hatakiwi kuachia pumzi katikati ya msukumo
· 9. Na anapoambiwa kusukuma anatakiwa kusukuma kwa
nguvu zote
· 9. Mama mjamzito anatakiwa Kuwa msikivu na mwerevu
wakati wa uchungu pia toa ushirikiano kwa mkunga.
Hivi vitu vikifanyika na
kuzingatiwa wakati wa uchungu basi
kipindi hiki cha uchungu kinaweza kutuletea matokeo mazuri ya
ujauzito na
matokeo mazuri ya ujauzito ni yale yanayo ambatana na
kujifungua salama kwa
afya ya mama na mtoto pia bila kuwa na
matatizo yoyote.
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR
MLALO
REFERENCES
D.C.DUTTA, (2011) Text book of
obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON
GORDON W.GARLAND and ROSEMARY
C. PERKES, (1959) a text book for pupil midwives, The English universities
press ltd, LONDON.
LINDA K. BROWN and V.RUTH
BENNETH, (1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, Churchill Livingstone,
EDINBURGH LONDON
Asante kwa elimu nzuri
ReplyDelete