DALILI HATARISHI KWA AFYA YA MTOTO MCHANGA.

 Mtoto mchanga ni nani?

Mtoto mchanga ni mtoto mwenye umri wa siku 28 baada ya 

kuzaliwa, afya ya mtoto mchanga huzidi kuimalika kadri 

anavyozidi kukuwa.

mtoto mchanga anapokuwa na tatizo lolote la ki-afya au 

anapokuwa anaumwa, ni vigumu kwa mzazi au mlezi 

kufahamu kwasababu mtoto hawezi ongea anachohisi mwilini 

mbali huyu mtoto ataonyesha ishara au dalili zinazoashilia 

kuwa kuna kitu mwilini kinamsumbua na angependa 

kupatiwa msaada.



hivyo basi ni jukumu la mzazi au mlezi kuweza kuzifahamu 

hizo dalili ili aweze kuzitambua kipindi pale mtoto 

atakapozionyesha, hizi ni baadhi ya hatarishi ambazo 

zikionekana kwa mtoto basi huashiria kuwa mtoto anaumwa 

au anashida na angependa kupewa huduma ya afya.



  • kutokuwa na hamu ya chakula au kukataa kula chakula
  • mwili wake kupata joto kali
  • kupata dege dege
  • kupoteza fahamu
  • kupumua kwa haraka/kupumua kwa shida
  • kutohisi kitu chochote, mfano akishituliwa
  • kutoa sauti akiwa ana pumua
  • kuwa wa baridi sana
  • mwili wake kuwa wa njano
  • kutopata choo ndani ya masaa 24
  • kulia bila sababu inayoweza kujulikana
  • uso wake kuwa wa bluu
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO AFISA MKUNGA

FERERENCES
www.parents.com
www.momjunction.com
www.livestrong.com
www.thebump.com
www.babycenter.com

No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.