MAAMBUKIZI YA CORONA VIRUSI KWA MAMA-MJAMZITO

 

Mwanamke akipata ujauzito kinga yake ya mwili hubadilika na 

kuwa chini hivyo kumuweka katika hatari ya kupata magonjwa 

mbalimbali katika kipindi cha ujauzito, wanasayansi wanasema 

kuwa mabadiliko ya kinga ya mwili yanayotokea katika kipindi 

cha ujauzito yanamuweka mama-mjamzito katika hatari kubwa 

ya kupata maambukizi ya virusi vya corona kuliko mama asiye 

mjamzito, pia mama- mjamzito yupo mwenye maambukizi ya 

virusi vya corona yupo katika hatari ya kujifungua kabla ya umri 

wa mimba wa kujifungua. 


 

Wanasayansi wanaendelea kuchunguza kwa kina kirusi cha 

corona na madhara yake kwa ujauzito, lakini kwa sasa ni vyema 

mama-mjamzito akachukua tahadhari ya kujikinga na 

maambukizi ya virusi vya corona kwa

  • ·         kunawa mikono na sabuni/sanitizer
  • ·         kuvaa barakoa usoni kwa kufunika mdomo na pua
  • ·         kujiepusha na misongamano ya watu wengi

IIIIMETAFISIRIWA NA BARAKA EDGAR MLALO, AFISA MKUNGA, KUTOKA KWENYE TOVUTI YA www.cdc.gov



No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.