DALILI ZA UJAUZITO


Mwanamke akipata ujauzito mwili wake hupatwa na mabadiliko 

ambayo haya mabadiliko huweza tumika kama dalili za ujauzito 

japokuwa sio kila hayo mabadiliko huashilia kuwa mwanamke ni 

mjamzito, hivyo basi mwanamke akishaona baadhi ya mabadiliko 

hana budi kupima uwepo wa ujauzito ili aweze kuthibitisha kama 

kweli ni mjamzito.
                               
Hizi ni baadhi ya dalili za mapema ambazo huweza mtokea 

mwanamke hivyo kumpa wasiwasi kama ni mjamzito.

Ø 1. Kutopata hedhi(damu) ya mwisho wa mwezi
               
                       
Ø 2. Matiti kujaa au kuvimba

3. Matiti kutoa maji maji(maziwa)

     4. Kichefuchefu

    5. Kuchoka kwa mwili

    6. Kupatwa na ongezeko la haja ndogo

    7. Uso kutokwa na chunusi

8. Kutokwa na hamu ya kula

9. Kuchukia baadhi ya vyakula

10. Ongezeko la maji maji ya ukeni

Si lazima mwanamke akipatwa na baadhi ya hizo dalili hapo juu 

basi zinamaanisha  tayari ameshapata ujauzito, lakini akipata baadhi 

ya hizo dalili na akawa hajapata damu zake za mwisho wa mwezi 

basi hana budi kupima kipimo cha mimba na kuthibitisha uwepo wa 

ujauzito
                                                .
i
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO AFISA MKUNGA

REFERENCES.

D.C.DUTTA, (2011) Text book of obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON

GORDON W.GARLAND and ROSEMARY C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english  universities press ltd, LONDON.

LINDA K. BROWN and V.RUTH BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill livingstone, EDINBURGH LONDON

BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD, CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc GrawHill Education, UNITED STATES




No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.