DALILI ZA UJAUZITO
Mwanamke akipata ujauzito
mwili wake hupatwa na mabadiliko
ambayo haya mabadiliko huweza tumika kama
dalili za ujauzito
japokuwa sio kila hayo mabadiliko huashilia kuwa mwanamke ni
mjamzito, hivyo basi mwanamke akishaona baadhi ya mabadiliko
hana budi kupima
uwepo wa ujauzito ili aweze kuthibitisha kama
kweli ni mjamzito.
Hizi ni baadhi ya dalili za
mapema ambazo huweza mtokea
mwanamke hivyo kumpa wasiwasi kama ni mjamzito.
Ø 1. Kutopata hedhi(damu) ya mwisho wa mwezi
Ø 2. Matiti kujaa au kuvimba
3. Matiti kutoa maji maji(maziwa)
4. Kichefuchefu
5. Kuchoka kwa mwili
6. Kupatwa na ongezeko la haja ndogo
7. Uso kutokwa na chunusi
8. Kutokwa na hamu ya kula
9. Kuchukia baadhi ya vyakula
10. Ongezeko la maji maji ya ukeni
Si lazima mwanamke akipatwa na
baadhi ya hizo dalili hapo juu
basi zinamaanisha tayari ameshapata ujauzito, lakini akipata baadhi
ya hizo dalili na akawa hajapata damu zake za mwisho wa mwezi
basi hana budi
kupima kipimo cha mimba na kuthibitisha uwepo wa
ujauzito
.
i
IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR
MLALO AFISA MKUNGA
REFERENCES.
D.C.DUTTA, (2011) Text book of
obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON
GORDON W.GARLAND and ROSEMARY
C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english universities press ltd, LONDON.
LINDA K. BROWN and V.RUTH
BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill
livingstone, EDINBURGH LONDON
BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD,
CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc
GrawHill Education, UNITED STATES
No comments