MIMBA

Mimba ni hali ya kubeba kijusi/vijusi vinavyokuwa na kuendelea 

tumboni mwa mwanamke. 

Mimba hutokea au hupatikana pale tu yai la kike na mbegu ya 

mwanaume kukutana na kutengeneza kijusi ambacho hukaa kwenye 

tumbo la uzazi mpaka pale kitakapotolewa nje ya tumbo la uzazi 

kama mtoto mchanga, katika kipindi hiki mwanamke hapati damu 

zake za mwezi kwa muda wa takribani wiki 40 sawa na siku 280.


                       
Mwanamke alie na mimba huitwa mama mjamzito au mjamzito, 

katika kipindi hiki mama mjamzito hupata mabadiliko ya kimwili na 

kiakili pia.
                       



Ujauzito umegawanyika katika vipindi vitatu, kipindi cha kwanza 

kinachoanza wiki 0-12, kipindi cha pili wiki13-28 na kipindi cha 

tatu wiki 29 hadi kujifungua.


                       
Katika kila vipindi vya ujauzito kuna mabadiliko ambayo hutokea 

kwenye kila kipindi ambayo hayo mabadiliko hutumika kama dalili 

za ujauzito




IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO (AFISA MKUNGA)


D.C.DUTTA, (2011) Text book of obstetrics, seventh edition, new central book agency (P) ltd, LONDON

GORDON W.GARLAND and ROSEMARY C. PERKES,(1959) A text book for pupil midwives, The english  universities press ltd, LONDON.

LINDA K. BROWN and V.RUTH BENNETH,(1999) Myles textbook for midwives, thirteenth edition, churchill livingstone, EDINBURGH LONDON

BLOOM SPONG, CASEY SHEFFIELD, CUNNINGHAM LEVENO and DASHE HOFFMAN, (2014) WILLIAMS OBSTETRICS 24 EDITION, Mc GrawHill Education, UNITED STATES



No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.