KIFAFA CHA MIMBA

 Ni hali ambayo huweza kumtokea mama-mjamzito wenye 

umri wa miezi mitano sawa na wiki 20, mwenye msukumo wa 

damu mkubwa wa kuanzia 140/90mmHg na zaidi, ambapo 

mama-mjamzito mwenye huu msukumo wa damu huanguka 

kifafa mara moja au zaidi, hii hali hutokea kipindi cha ujauzito 

au ndani ya siku 42 baada ya kujifungua.



hali hii ya kupata kifafa kipindi cha ujauzito husababishwa na 

msukumo wa damu kuwa mkubwa ambao haujatibiwa na 

kama hautagundulika mapema na kuachwa kutibiwa 

husababisha mama mjamzito kupata kifafa na kama hatua za 

kumtibu hazitachukulika husababisha kifo kwa mtoto na 

mama pia.


lakini si kila mama-mjamzito mwenye msukumo wa damu 

mkubwa (pressure) anaweza kupata kifafa cha mimba, ila hali 

hii humuweka mama mjamzito katika hatari ya kupata kifafa 

cha mimba kama hatogundulika na kupewa huduma mapema.

hivyo basi ni vyema kufanya uchunguzi mapema kuhusu afya 

ya mama mjamzito ili kuweza kuelewa kama msukumo wa 

damu ni mkubwa na kama unahitaji matibabu na kwa wale 

wanawake wanaojifahamu kuwa wana shinikizo la damu ni 

vyema kuonana na watoa huduma za afya ili kuweza kuchukua 

hatua sitahiki za kujilinda na kifafa cha mimba.

Hivyo basi uhudhuriaji wa kliniki ya wajawazito ni muhimu sana 

IMEANDALIWA NA BARAKA EDGAR MLALO, AFISA MKUNGA

No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.