JINSI YA KUTUMIA P2 - MATUMIZI YA P2

 Matumizi ya P2 hutegemea na aina ya njia ya dharura unayotumia, 

kuna aina mbili zinazotumika kama njia za dharura za uzazi wa 

mpango.

1. vidonge

2. kitanzi

vidonge ndo njia inayotumika sana kuliko kitanzi, hizi njia zote 

ufanisi wake unapungua mara baada ya masaa 120 (siku 5) kupita 

bila kutumika, maana yake njia za dharura za uzazi wa mpango 

zinatakiwa kutumika ndani ya masaa 120 (siku 5) baada ya dharura 

kutokea na ufanisi unaongezeka zaidi kama zitatumuka ndani ya 

masaa 72 (siku3) baada ya dharura kutokea.

kitanzi hutakiwa kuwekwa ndani ya masaa 120 (siku 5) baada ya 

dharura kutokea, utumiaji wa kitanzi baada ya masaa 120 (siku 5) 

huambatana na kutozuia mimba, hivyo basi unashauriwa kutumia 

njia hii ndani ya muda muafaka.

vidonge hutakiwa kutumika ndani ya masaa 120 (siku 5) baada ya 

dharura kutokea, ufanisi wa utendaji kazi wake huongezeka zaidi 

vinapotumiaka mapema baada ya dharura kutokea.

vidonge hivi hupatikana madukani vikiwa katika aina tofauti, 

hupatikana kikiwa kidonge kimoja, ambacho humezwa mara moja.

vikiwa vidonge viwili, ambavyo humezwa mara mbili, kimoja baada 

ya dharura na cha pili baada ya masaa kumi na mbili (12). 

pia vidonge vya majira vya uzazi wa mpango vinaweza kutumika 

kama njia ya dharura ya uzazi wa mpango, ambapo mtumiaji 

anatakiwa kumeza jumla vidonge nane (8) ndani ya siku moja. 

baada ya dharura anatakiwa kumeza vidonge vinne (4) na baada ya 

masaa kumi na mbili (12) anamalizia vinne (4) vilivyobaki.












No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.