MADHARA YA MATUMIZI YA P2

Vidonge vya dharura ya uzazi wa mpango au P2 havina madhara  

kwa mtumiaji endapo tu vitatumika ipasavyo. matumizi ya P2 

yanatakiwa yatumike pale tu dharura inapotokea, P2 haitakiwi 

kutumika kama njia ya uzazi wa mpango, bali inatakiwa itumike 

kama njia ya dharura ya uzazi wa mpango. 

ni vyema kutumia njia zingine za uzazi wa mpango kama una lengo 

la kutopata ujauzito na sio kutengemea P2. njia hizi za uzazi wa 

mpango ni kama vile sindano, vidonge, kitanzi, jiti na condom.

matumizi holela ya P2 huweza ambatana na mvurugiko wa 

mzunguko wa hedhi (hormone imbalance) hivyo kuleta usumbufu 

katika upatikanaji wa mimba kwa wakati itakapohitajika. pia 

matumizi holela ya P2 humuweka mteja katika hatari ya kupata 

maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama vile UKIMWI, 

KASENDWE NA KISONONO.

pia matumizi ya P2 huambatana na maudhi kama vile vichomi, 

kichefuchefu, matone ya damu, matiti kujaa, kutapika, uchovu wa 

mwili, mvurugiko wa mzunguko wa hedhi, maumivu ya tumbo, 

maumivu ya kichwa. hizi dalili ni za kawaida na si madhara kwa 

mtumiaji wa P2 na hupotea zenyewe bila matumizi ya dawa.

matumizi sahihi ya P2 humsaidia mtumiaji asipate mimba na asipate 

madhara yoyote yanayosababishwa na P2, hivyo unashauliwa 

kutumia P2 wakati wa dharura tu na sio kila utakapofanya tendo la 

ndoa,














No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.