MADHARA YA MATUMIZI YA P2

  • Vidonge vya dharura ya uzazi wa mpango au P2 havina madhara  kwa mtumiaji endapo tu vitatumika ipasavyo. matumizi ya P2 yanatakiwa yatumike pale tu dharura inapotokea, P2 haitakiwi kutumika kama njia ya uzazi wa mpango, bali inatakiwa itumike kama njia ya dharura ya uzazi wa mpango. 

                                                     

  • Ni vyema kutumia njia zingine za uzazi wa mpango kama una lengo la kutopata ujauzito na sio kutengemea P2. njia hizi za uzazi wa mpango ni kama vile sindano, vidonge, kitanzi, jiti na condom.

                                                    

  • Matumizi holela ya P2 huweza ambatana na mvurugiko wa mzunguko wa hedhi (hormone imbalance) hivyo kuleta usumbufu katika upatikanaji wa mimba kwa wakati itakapohitajika. pia matumizi holela ya P2 humuweka mteja katika hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama vile UKIMWI, KASENDWE NA KISONONO.

                                                  

  • Pia matumizi ya P2 huambatana na maudhi kama vile vichomi, kichefuchefu, matone ya damu, matiti kujaa, kutapika, uchovu wa mwili, mvurugiko wa mzunguko wa hedhi, maumivu ya tumbo, maumivu ya kichwa. Hizi dalili ni za kawaida na si madhara kwa mtumiaji wa P2 na hupotea zenyewe bila matumizi ya dawa. Matumizi sahihi ya P2 humsaidia mtumiaji asipate mimba na asipate madhara yoyote yanayosababishwa na P2, hivyo unashauliwa kutumia P2 wakati wa dharura tu na sio kila utakapofanya tendo la ndoa,



WASILIANA NASI KWA UFAHAMU ZAIDI +255757599024-what's app.










No comments

Theme images by compassandcamera. Powered by Blogger.